Unordered List


Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Saturday, 6 June 2015

'Umaanawi wa mfumo wa Kiislamu Iran ni wa kipekee'

Ayatullah Mohammad Imami Kashani Ayatullah Mohammad Imami Kashani
Khatibu wa Sala ya Ijumaa mjini Tehran amesema mfumo wa Kiislamu wa Iran ni wa kipekee duniani kutokana na umaanawi wake. Ayatullah Mohammad Imami Kashani, khatibu wa muda wa sala ya Ijumaa wiki hii Tehran ameashiria umuhimu na nafasi ya mfumo wa Kiislamu wa Iran na tafauti yake na mifumo mingine duniani na kusema: "Sira ya kivitendo ya Imam Khomeini MA, muasisi wa Jamhuri ya Kiislamu ni yenye thamani kubwa sana ambayo inapaswa kuzingatiwa na  jamii hasa kizazi cha vijana." Ayatullah Imami Kashani aidha ameashiria namna Imam Khomeini MA alivyolipatia umuhimu suala la umoja wa ulimwengu wa Kiislamu na kusema: "Umoja wa Waislamu, uchumi, maisha bora ya wananchi, na kumfahamu adui ni kati ya nukta muhimu katika sira ya kivitendo ya Imam." Ameongeza kuwa sira ya kivitendo ya Imam Khomeini MA haiwezi kamwe kupotoshwa. Khatibu wa Sala ya Ijumaa ameongeza kuwa: 'Baada ya kuaga dunia Imam Khomeini MA, uwepo wa Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Khamenei, ni neema kubwa kwa Jamhuri ya Kiislamu. Wilaya au uongozi wake ni muhimu sana kwa mfumo na jamii a Kiislamu kwa sababu anafuata ile ile njia ya Imam Khomeini MA."  Ayatullah Kashani ameashiria nafasi ya 'Faqihi Mtawala' au Wilayat Faqih katika mfumo wa Kiislamu na kusema wale ambao wanatilia shaka utawala huo ni maadui wa mfumo wa Kiislamu.  Khatibu wa Muda wa Sala ya Ijumaa sambamba na kuelezea matumaini yake kuwa kadhia ya nyuklia itatatuliwa sambamba na kuhifadhiwa haki za taifa la Iran, ametoa wito kwa timu ya Iran katika mazungumzo ya nyuklia kulinda haki za taifa hili

No comments:

Post a Comment