Unordered List


Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Saturday, 6 June 2015

Mikutano ya siri ya Saudia na Israel kuhusu Iran

Anwar Majed Eshki (kushoto) kutoka Saudia na Dore Gold wa Israel Anwar Majed Eshki (kushoto) kutoka Saudia na Dore Gold wa Israel
Ripoti imefichuka kuhusu mikutano kadhaa ya siri baina ya wawakilishi wa Saudi Arabia na Israel kwa lengo la kujadili misimamo yao kuhusu Iran.
Kwa mujibu wa tovuti ya Bloomberg, mikutano hiyo imefanyika mara tano katika kipindi cha miezi 17 iliyopita ambapo maafisa hao wa Saudia na utawala haramu wa Israel wamekutana nyakati mbali mbali huko India, Italia na Jamhuri ya Czech.
Tovuti hiyo imenukulu jenerali mstaafu katika jeshi la Israel aliyeshiriki katika moja ya vikao hivyo akisema, "Tuligundua kuwa tunakabiliana na matatizo na changamoto za pamoja na pia baadhi ya majibu ya pamoja." Aidha siku ya Alkhamisi maafisa mashuhuri wa zamani wa Saudia na Israel walikutana katika taasisi za Council on Foreign Relations huko Washington. Kikao hicho kilihudhuriwa na Anwar Majed Eshki, mshauri wa zamani wa serikali ya Saudia, na Dore Gold balozi wa zamani wa Israel aliye karibu na Waziri Mkuu wa Utawala wa Kizayuni Benjamin Netanyahu. Israel na Saudia zote kwa pamoja zinapinga kile zinachosema ni kuenea ushawishi wa Iran katika eneo. Aidha pande mbili hizo zimetangaza wazi kupinga mapatano ya nyuklia baina ya Iran na madola sita makubwa duniani. Hivi karibuni pia gazeti moja la Uingereza lilisema Israel imetangaza kuwa tayari kuipa Saudia makombora katika vita vyake dhidi ya watu wa Yemen

No comments:

Post a Comment