Unordered List


Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Saturday, 6 June 2015

Marekani yapinga Kagame kugombea muhula wa 3

Paul Kagame Paul Kagame
Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani imesema haiungi mkono rais wa Rwanda, Paul Kagame kugombea tena muhula wa tatu kwenye uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika mwaka 2017. Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani anayehusika na masula ya Afrika amewambia waandishi wa habari mjini Washington kuwa, Rwanda inahitaji kuwa na taasisi zenye nguvu zitakazosimamia uimarishwaji wa demokrasia na wala haihitaji mtu mwenye nguvu kufanya kazi hiyo.
Siku chache zilizopita, wabunge wa Rwanda walifichua kwamba, mamilioni ya Wanyarwanda wamemuomba Rais Paul Kagame kuendelea kuwaongoza hata baada ya 2017. Kwa msingi huo, wabunge hao wamesema watachunguza kwa makini maombi hayo ya wananchi na iwapo yatakuwa na uzito, wataanza mchakato wa kubadilisha katiba ili kuondoa kifungu kinachoweka kikomo kwa muhula wa rais kuongoza. Kwa sasa katiba ya Rwanda inasema rais anayechaguliwa hawezi kuzidisha zaidi ya mihula miwili madarakani

No comments:

Post a Comment