Unordered List


Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Saturday, 6 June 2015

Waliokufa katika mlipuko Ghana wafika hadi 175

Habari kutoka Ghana zinasema kuwa, idadi ya watu waliofariki dunia kufuatia moto uliotokea katika kituo kimoja cha mafuta katika mji mkuu Accra imepanda na kufikia 175. Duru za hospitali zinasema watu wengi waliokimbizwa kwenye vituo vya matibabu wakiwa na majeraha mabaya ya moto wamefariki dunia kati ya jana usiku na leo mchana. Mlipuko huo ulitokea siku ya Jumatano wakati mamia ya watu walipokuwa wamejihifadhi katika kituo cha mafuta kutokana na mvua kubwa zilizokuwa zikinyesha. Tarayi Ghana imetangaza siku tatu za maombolezo ya kitaifa kufuatia vifo hivyo. Rais John Dramani Mahama ambaye ametemelea eneo la mkasa huo amesema taifa limetikiswa na idadi kubwa ya watu waliopoteza maisha kwenye mlipuko huo.
Mvua za masika zinazoendelea kunyesha huko Ghana zimesababisha nyumba nyingi kuharibika na hivyo kuwaacha watu wengi bila makao. Wizara ya Afya ya nchi hiyo imetahadharisha

No comments:

Post a Comment