Unordered List


Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Sunday, 14 June 2015

Bush amtaka Obama atume wanajeshi wa US Iraq

Rais wa zamani wa Marekani George W. Bush amemkosoa Rais wa nchi hiyo Barack Obama kutokana na stratijia anayotumia katika vita dhidi ya kundi la kigaidi na kitakfiri la Daesh (ISIL) na kusema kuwa Washington inapaswa itume wanajeshi wake nchini Iraq. Bush amesema msimamo wake ni kwamba kuna haja ya kutuma vikosi vya nchi kavu nchini Iraq. Bush amedai kuwa serikali yake iliushinda mtandao wa kigaidi wa al-Qaeda wakati ilipotuma askari wa ziada nchini Iraq. Barack Obama amekuwa akilaumiwa vikali kwa kushindwa kulisambaratisha kundi la kigaidi na kitakfiri la Daesh katika nchi za Iraq na Syria. Mapema wiki hii Obama alikiambia kikao cha nchi tajiri zinazounda kundi la G7 kilichofanyika nchini Ujerumani kwamba hawajawa na stratijia iliyokamilika dhidi ya Daesh. Tangu mwaka uliopita serikali ya Washington imekuwa ikiongoza operesheni za mashambulio ya anga dhidi ya ngome za kundi la kigaidi na kitakfiri la Daesh lakini mashambulio hayo hayajapata mafanikio yoyote. Siku ya Jumatano iliyopita, msemaji wa Ikulu ya Marekani Josh Earnest alisema Rais Obama ametoa amri ya kutumwa askari 450 wa ziada nchini Iraq kwa ajili ya kutoa ushauri kwa vikosi vya nchi hiyo kutokana na ombi la Waziri Mkuu Haidar al-Abadi. Askari hao wataifanya idadi ya askari wote wa Marekani walioko nchini Iraq ifikie 3,550. Kwa mujibu wa Wizara ya Ulinzi ya Marekani Pentagon, hadi sasa nchi hiyo imeshatumia zaidi ya dola bilioni 2.7 katika operesheni za kijeshi dhidi ya Daesh katika nchi za Iraq na Syria ambazo ni wastani wa zaidi ya dola milioni tisa kwa siku…/

No comments:

Post a Comment