Unordered List


Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Saturday, 6 June 2015

Saudia yaendeleza jinai zake nchini Yemen

Nyumba za raia zilizoharibiwa katika hujuma ya Saudia Yemen Nyumba za raia zilizoharibiwa katika hujuma ya Saudia Yemen
Saudi Arabia imeendeleza jinai zake za kivita nchini Yemen huku makumi ya raia wasio na hatia wakiuawa katika hujuma za leo.
Kwa mujibu wa shirika rasmi la habari la Yemen, Saba, katika hujuma ya ndege za kivita za Saudi Arabia leo Ijumaa katika maeneo mbali mbali ya Yemen hasa mikoa ya Sa'ada, Hajja na Aden, raia wasiopingua 40 wameuawa na wengine kadhaa kujeruhiwa.  Ndege za kivita za Saudi Arabia pia zimedondosha mabomu katika hospitali katika mji wa Dhamar mbali na kuhujumu pia chuo kikuu mjini humo.
Huku hayo yakijiri makumi ya maelfu ya watu wameandamana katika mji mkuu wa Yemen, Sana'a kupinga na kulaani hujuma ya kijeshi ya Saudi Arabia dhidi ya nchi yao.
Kwa mujibu wa ripoti ya hivi karibuni ya Taasisi ya Uhuru ya Yemen, tangu yalipoanza mashambulio ya kivamizi ya Saudia dhidi ya nchi hiyo Machi 26 mwaka huu ambayo yamefanywa bila ya idhini ya Umoja wa Mataifa, hadi sasa watu wasiopungua 4,000 wameshauawa na wengine 7,000 kujeruhiwa.  Aghalabu ya wahanga wa hujuma hizo zinazoongozwa na Saudia ni watoto, wanawake na raia wa kawaida wasio na hatia

No comments:

Post a Comment