Unordered List


Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Sunday, 14 June 2015

Askari wa Israel wamuua shahidi Mpalestina Ramallah

Askari wa utawala haramu wa Israel wamempiga risasi na kumuua shahidi Mpalestina katika kijiji kimoja karibu na mji wa Ramallah katika Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan.
Abdullah Ghanayem aliyekuwa na umri wa miaka 21 aliuawa shahidi katika Kijiji cha Kufor Malek mapema leo asubuhi.
Duru za Palestina zinadokeza kuwa gari la kijeshi la Israel limepinduka katika makabaliano hayo na kumuangukia Mpalestina aliyeuawa shahidi.
Askari wa Israel wamekihujumu kijiji hicho na kuwateka Wapalestina kadhaa. Jeshi la utawala dhalimu wa Israel huvamia nyumba za Wapalestina mara kwa mara katika Ukingo wa Magharibi na kuwateka nyara Wapalestina ambao hupelekwa katika korokoro za kuogofya za utawala huo.

No comments:

Post a Comment