Unordered List


Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Sunday, 14 June 2015

Yemen: Saudia inatumia silaha zilizopigwa matukufu

Wizara ya Afya ya Yemen imetangaza kuwa Saudi Arabia imetumia silaha zilizopigwa marufuku kimataifa dhidi ya wananchi wa Yemen katika mashambulio yake ya kijeshi katika nchi hiyo ya Kiarabu. Tamim Shami Msemaji wa Wizara ya Afya ya Yemen ameeleza kuwa baadhi ya watu waliojeruhiwa katika mashambulizi ya Saudia wana dalili zinazoashiria kwamba wameathiriwa na silaha ziliopigwa marufuku zilizodondoshwa na ndege za Saudi Arabia katika mashambulizi yake katika mji mkuu wa Yemen Sana’a yaliyoanza Machi 26 mwaka huu pasina kuidhinishwa na Umoja wa Mataifa.  
Msemaji wa Wizara ya Afya ya Yemen ameongeza kuwa nchi hiyo inasumbuliwa na hali inayozidi kuwa mbaya ya kibinadamu kutokana na kuwepo uhaba wa suhula za tiba. Amesema watu zaidi ya 5,000 wanaugua homa ya dengue na malaria. 

No comments:

Post a Comment