Unordered List


Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Sunday, 14 June 2015

Misri yafungua tena kivuko cha mpakani cha Rafah

Serikali ya Misri leo imekifungua tena kivuko cha Rafah kilichoko kwenye mpaka wa pamoja wa nchi hiyo na Ukanda wa Gaza ili kuwaruhusu Wapalestina kuingia na kutoka katika eneo hilo, ikiwa ni mara ya kwanza katika kipindi cha miezi mitatu, katika kile kinachoonekana kama ishara ya kupungua mvutano uliokuwepo kati ya Cairo na Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS iliyoshika hatamu za eneo la Gaza. Ukanda wa Gaza umewekewa mzingiro na utawala wa Kizayuni wa Israel kwa zaidi ya mwaka wa saba sasa, na serikali ya Misri imekuwa ikikifunga kivuko cha Rafah kwa muda mwingi tangu Rais Mohammad Morsi aliyekuwa na uhusiano wa karibu na Hamas alipoondolewa madarakani mwaka 2013. Wiki mbili zilizopita Cairo ilikifungua kituo cha Rafah kwa muda wa siku tatu kuruhusu safari za upande mmoja tu kwa Wapalestina waliokuwa wamekwama nje ya Ukanda wa Gaza kuweza kurejea makwao katika eneo hilo. Lakini hatua ya leo ya kuruhusu kuingia na kutoka Gaza kupitia kivuko cha Rafah inaonekana kama ishara ya kuboreka uhusiano wa Misri na Hamas baada ya msuguano na mvutano mkali uliokuwepo kwa muda wa miaka miwili. Serikali ya Cairo imeituhumu Hamas kuwa inayaunga mkono makundi ya wanamgambo wenye silaha yanayopambana na serikali ya Misri katika Rasi ya Sinai, tuhuma ambazo Hamas imezikadhibisha. Maafisa katika mpaka wa Misri na Palestina inayokaliwa kwa mabavu wamesema kivuko cha Rafah kitaendelea kuwa wazi kwa muda wa siku tatu, huku baadhi ya duru za Palestina zikieleza kwamba muda huo unaweza kuongezwa; hata hivyo hakuna kauli yoyote iliyotolewa na maafisa wa Misri kuthibitisha suala hilo…

No comments:

Post a Comment