Unordered List


Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Sunday, 14 June 2015

Iran yatoa radiamali kupinga taarifa ya PGCC

Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amepinga taarifa ya hivi karibuni ya Baraza la Ushirikiano la Ghuba ya Uajemi kuhusu visiwa vitatu vya Iran. Bi Marzieh Afkham amejibu matamshi hayo ya Baraza la Ushirikiano la Ghuba ya Uajemi kwa kusema kuwa: Kukaririwa madai yasiyo na msingi hakujakuwa na athari kwa uhakika wa kihistoria. Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema visiwa vya Bumusa, Tomb Kubwa na Ndogo ni sehemu ya ardhi ya Iran isiyoweza kutenganishwa. Afkham ameongeza kuwa:  Iran inatoa kipaumbele katika siasa zake kwa suala la kuwa na uhusiano mwema na majirani zake, uhusiano ambao umejengeka kwa kutoingilia masuala ya nchi nyingine na kuheshimiana pande mbili na haina kizuizi chochote katika kustawisha na kupanua mahusiano ya kirafiki. Bi Afkham amesema Iran inakaribisha kuwepo maelewano na ushirikiano mkubwa wa pande zote na majirani zake

No comments:

Post a Comment