Unordered List


Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Saturday, 6 June 2015

Kenya yawaonya wafanyamagendo ya pembe za ndovu

Rais Uhuru Kenyatta Rais Uhuru Kenyatta
Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya ametahadharisha maafisa wa serikali yake wanaojihusisha na biashara haramu ya pembe za ndovu akisema watakamatwa na kufikishwa mbele ya vyombo vya sheria. Akizungumza mapema leo kwenye mkutano wa wawekezaji mjini Nairobi, Rais Kenyatta ameagiza maafisa wa usalama kuchunguza kesi inayohusiana na kukamatwa kwa shehena kubwa ya pembe za ndovu huko Thailand mwezi Aprili ambayo inaaminika kutoka Kenya na kuwafikisha wahusika wote mbele ya vyombo vya sheria. Pia Rais wa Kenya ameonya wawekezaji na maafisa wa idara za serikali wanaojihusisha na uingizaji wa bidhaa bandia nchini akisema chuma chao ki motoni. Kiongozi huyo amesema bidhaa bandia zinazoingizwa Kenya zinachangia soko la ndani kuporomoka na hivyo kuwafanya vijana wengi kukosa nafasi za ajira. Pia amesema jmbo hilo linahatarisha usalama wa taifa kwani bidhaa ghushi zinazoingizwa hazikaguliwi na hivyo kuna uwezekano wa kuingizwa hata silaha kupitia njia hizo.
Maafisa kadhaa wa idara ya forodha pamoja na wale wa mamlaka ya ukusanyaji ushuru wamekamatwa na kufikishwa kortini kuhusiana na biashara haramu ya meno ya tembo

No comments:

Post a Comment