Unordered List


Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Monday, 29 June 2015

Upigaji kura waanza nchini Burundi, ghasia zaripotiwa

Zoezi la upigaji kura linaendelea nchini Burundi na tayari kumeripotiwa kutokea mashambulizi katika vituo kadhaa vya kupigia kura.
Wapiga kura wanaripotiwa kuwa wachache katika uchaguzi huo wa bunge na serikali za mitaa huku watu wengi wakionekana kuhofia kujitokeza katika vituo vya kupigia kura. Uchaguzi huo unafanyika pamoja na kuwa jamii ya kimataifa imeitaka serikali ya Burundi kuuahirisha na kupanga wakati mwingine unaokubalika na pande zote husika na chaguzi nchini humo.
Wapinzani Burundi wametangaza kususia uchaguzi kwa madai kuwa si huru na wa haki. Burundi ilitumbukia katika mgogoro mkubwa wa kisiasa kuanzia mwezi Aprili wakati Rais Pierre Nkurunziza alipotangaza uamuzi wake wa kugombea kiti cha urais kwa muhula wa tatu. Zaidi ya watu 70 wamepoteza maisha katika machafuko ya kabla ya uchaguzi Burundi huku wengine zaidi ya laki moja wakikimbia nchi

Monday, 22 June 2015

ZANZIBA MPYA KATIKA CCTV

Mji Mkongwe wafungwa CCTV




Katibu wa Kamati ya Wataalamu ya usimamizi wa Mradi wa CCTV Camera Nd. Jabir Haji Abdulla akionyesha picha mbali mbali zinazonaswa na kurikodiwa katika maeneo mbali mbali ya Mji Mkongwe.

Zanzibar inatarajia kuimarika zaidi kiulinzi na kiusalama sambamba na kuongeza mapato yake kupitia sekta ya utalii baada ya kukamilika kwa mradi muhimu wa Kamera za  kurikodi matukio mbali mbali ya kila siku { CCTV CAMERA } zinazofungwa katika eneo la Mji Mkongwe wa Zanzibar.

Mradi huo muhimu wa Camera uliofadhiliwa na Kampuni ya Kimataifa ya Mtandao wa Mawasiliano ya Kisasa ya ZTE yenye Makao Makuu yake Nchini  Jamuhuri ya Watu wa China umekuja Zanzibar kufuatia ziara ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi aliyoifanya Nchini China mwisho mwa mwaka uliopita.



Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi alipata fursa ya kukagua Kituo cha mradi huo { Comanding Post } kiliopo Malindi Mjini Zanzibar na kujionea Teknolojia mpya itakayotumika katika kuziongoza Kamera hizo.

Katibu wa Kamati ya Wataalamu ya usimamizi wa Mradi wa CCTV Camera Nd. Jabir Haji Abdulla alimueleza Balozi Seif kwamba mradi huo unatarajiwa kuwa na Carema 300 lakini zitakazofungwa kwa sasa ni Kamera 150 ambapo hadi sasa Kumi tayari zimeshafungwa.

Nd. Jabir alisema Kituo hicho  kitakachokuwa chini ya uangalizi  wa Idara zote za ulinzi Nchini  likiwemo Jeshi la Polisi, usalama wa Taifa, KMKM hivi sasa tayari kina uwezo kamili wa kurikodi matukio mbali mbali yanayotokea katika eneo la Mji Mkongwe.


Mounekano wa Picha tofauti zinazochukuliwa na kunaswa katika kituo cha kuongozea Camera za CCTV Malindi Mjini Zanzibar.

Katibu huyo wa Kamati ya Wataalamu ya usimamizi wa mradi huo alieleza kwamba Kamera za mradi huo zenye uwezo wa kuvuta tukio kwa zaidi ya mita 150 zitasaidia kurikodi matukio mbali mbali kama ujambazi, makosa ya bara barani yanayofanywa na madereva wazembe pamoja na kuongoza misafara ya viongozi wakuu.

Alifahamisha kwamba katika kuimarisha hali ya usalama ndani ya Mji wa Zanzibar  upo mradi mwengine  unaotarajiwa kusimamiwa na Kampuni ya Zest utakaohusisha maeneo ya Bagharesa, Mlandege pamoja na Majengo ya Nyumba za Maendeleo Michezani.

“ Kamera hizi zenye uwezo wa kuzunguuka pembe zote { 360% }  zina uwezo wa kuvuta tukio lolote kwa zaidi ya Mita 150 na kuwa na vigezo vya kuufanya mji salama “. Alifafanua Katibu huyo wa Kamati ya Wataalamu ya Usimamizi wa CCTV.



Akitoa shukrani zake Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi aliipongeza Kampuni ya ZTE kwa jitihada ilizochukuwa za kutekeleza kwa vitendo ahadi iliyompa  kuanzisha mradi huo wakati wa ziara yake Nchini China.

Balozi Seif alisema Serikali ilipaswa kuwa na mradi huu muhimu kwa muda mrefu uliopita hasa ikilinganishwa na matukio mbali mbali yaliyowahi kutokea hapa nchini likiwemo la hujuma dhidi ya wageni wanaotembelea katika maeneo ya Utalii.

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar alielezea matumaini yake kwamba mradi huo kwa kiasi kikubwa utakapokamilika utasaidia kupunguza matukio tofauti ya uhalifu, ujambazi pamoja na ajali za kizembe zinazotokea bada barani.

Mradi  wa Kamera za  kurikodi matukio mbali mbali ya kila siku { CCTV CAMERA } ndani ya Mji wa Zanzibar umeripotiwa kuwa wa mwanzo kuwekwa ndani ya ukanda wa Afrika Mashariki

Thursday, 18 June 2015

Ramadhani imeanza leo maeneo mengi ya dunia

Waislamu katika nchi nyingi duniani leo wamenza funga ya mwezi Mtukufu wa Ramadhani.
Taasisi husika katika nchi mbalimbali za Kiislamu na zisizo za Kiislamu zilitangaza jana jioni kwamba Alkhamisi ya leo tarehe 18 Juni itakuwa siku ya kwanza ya mwezi wenye baraka na mtukufu wa Ramadhani ambamo Waislamu hufunga swaumu na kujikurubisha kwa Mola Karima kwa kujipinda kwa ibada na dua.
Hapa nchini Iran Ofisi ya Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ilitangaza jana jioni kwamba Leo Alkhamisi ni siku ya kwanza ya mwezi Mtukufu wa Ramadhani. Taarifa iliyotolewa na ofisi hiyo ilisema mwezi mwandamo ulionekana jana jioni na kwamba leo ni tarehe mosi Ramadhani.
Taasisi za kidini katika nchi kama Saudi Arabia, Misri, Sudan, Imarati na Qatar pia zimetangaza siku ya leo kuwa ni tarehe Mosi Ramadhani.
Leo Akhamisi pia imetangazwa kuwa tarehe Mosi Ramadhani katika nchi za Afrika Mashariki.
Idhaa ya Kiswahili ya Redio Tehran inawatakia Waislamu wote mwezi uliojaa baraka wa Ramadhani na tunamuomba Mola Karima atakabali dua na ibada zetu katika mwezi huu.

Monday, 15 June 2015

Magaidi wanaorudi kutoka Syria, Iraq ni hatari Balkan'

Shirika la Ubunifu la Mediterranean limeonya juu ya hatari ya kurejea magaidi katika eneo la Balkan kutoka katika nchi za Iraq na Syria. Mtandao wa Intaneti wa al Alam umelinukuu shirika hilo likisema hayo huko Sarajevo, Mji Mkuu wa Bosnia na kuongeza kuwa, hivi sasa kuna raia 115 wa Bosnia ndani ya kundi la kigaidi la Daesh katika nchi za Iraq na Syria. Kwa mujibu wa ripoti ya taasisi hiyo, eneo la Balkan linakabiliwa na hatari ya vitendo vya kigaidi kama vinavyoendelea hivi sasa huko Iraq na Syria kutokana na kurejea nyumbani raia wa nchi za eneo hilo waliopigana kwenye makundi ya kigaidi katika nchi hizo mbili za Kiarabu. Kwa mujibu wa shirika hilo, hatari hiyo inazikabili nchi zote za eneo la Balkan na hata Russia kutokana na baadhi ya raia wa nchi za Serbia, Albania, Macedonia na Montenegro kuwa na uhusiano wa karibu na makundi ya kigaidi kama vile Daesh. Takwimu za idara ya mahakama ya Bosnia zinaonesha kuwa karibu watu 192 wenye umri wa miaka 25 na vijana wenye umri wa kati ya miaka 15 hadi 17 wametembelea maeneo yenye mapigano huko Iraq na Syria kuanzia mwaka 2012 hadi mwishoni mwa mwaka jana. Shirika hilo limeitaka polisi ya Bosnia kuongeza nguvu za kudhibiti mitandao ya Intaneti na ya kijamii kwani ndiyo njia kuu inayotumiwa kuwashawishi vijana hao kujiunga na makundi ya kigaidi.

Sunday, 14 June 2015

Al-Shabaab wapanga hujuma Ramadhani Kenya

x'Al-Shabaab wapanga hujuma Ramadhani Kenya'
Kundi la kigaidi na kitakfiri la Al-Shabab linapanga njama ya kutekeleza mashambulizi nchini Kenya katika Mwezi Mtukufu wa Ramadhani. Hayo yamedokezwa na Inspekta Mkuu wa Polisi Kenya Joseph Boinnet. Akizungumza jana na waandishi habari jijini Nairobi, Bw Boinnet alisema kundi hilo la kigaidi limekuwa likipanga kutekeleza msururu wa mashambulizi katika mwezi Mtukufu wa Ramadhani ila halitaweza kwani serikali imegundua njama hiyo na usalama umeimarishwa. Ameongeza kuwa Al Shabab wanalenga kuhujumu taasisi za kiserikali, maduka, masoko, maeneo ya kidini, vyuo vya elimu, maafisa wa usalama na waandishi habari wanaoandika habari dhidi ya kundi hilo la kigaidi. Afisa mkuu wa polisi Kenya amesema, "Nawahakikishia ndugu na dada zetu Waislamu kuwa wataweza kutekeleza ibada za Ramadhani bila kuwepo pingamizi."
Aidha Boinnet ameonya kwamba wanachama wa al-Shaabab wanatumia mitandao ya kijamii kama vile Facebook, Twitter na WhatsApp kuwahadaa wananchi kwa kutumia akaunti fiche na blogu.
Kenya iko katika hali ya tahadhari kufuatia mauaji ya kigaidi yaliyotekelezwa mapema mwezi  Aprili na Al Shabab kwenye chuo kikuu cha Garrisa ambapo watu 148 waliuwawa na zaidi ya 70 kujeruhiwa

Askari wa Israel wamuua shahidi Mpalestina Ramallah

Askari wa utawala haramu wa Israel wamempiga risasi na kumuua shahidi Mpalestina katika kijiji kimoja karibu na mji wa Ramallah katika Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan.
Abdullah Ghanayem aliyekuwa na umri wa miaka 21 aliuawa shahidi katika Kijiji cha Kufor Malek mapema leo asubuhi.
Duru za Palestina zinadokeza kuwa gari la kijeshi la Israel limepinduka katika makabaliano hayo na kumuangukia Mpalestina aliyeuawa shahidi.
Askari wa Israel wamekihujumu kijiji hicho na kuwateka Wapalestina kadhaa. Jeshi la utawala dhalimu wa Israel huvamia nyumba za Wapalestina mara kwa mara katika Ukingo wa Magharibi na kuwateka nyara Wapalestina ambao hupelekwa katika korokoro za kuogofya za utawala huo.

Millicom (kampuni mama ya tiGO) yanunua hisa 85% Zantel

Wadau naona zantel kupitia hisa 85% za Et El Salat imenunuliwa na Millicom ambayo ni kampuni mama ya Tigo Tanzania.Ila jina la kampuni litabaki kama Zantel na vile vile Serikali ya Zanzibar itabaki na hisa zake 15% . Hongera Millicom sasa naona Tigo ikiwaaka.

============================== ==


Millicom has agreed to buy an 85 percent stake in Tanzanian operator Zanzibar Telecom (Zantel) from the Etisalat Group. Under the terms of the agreement, Millicom will pay a total cash consideration of USD 1 dollar and assume total debt obligations of USD 74 million.

In addition, Zantel will have up to USD 32 million in net current liabilities at closing.

Millicom expects the EBITDA of Zantel to reach USD 25 million through a combination of bringing new products and services to the existing customer base and delivering greater efficiencies. The acquisition agreement allows for an adjustment to the total consideration if that target is not reached by the end of 2019.

Millicom intends to retain and continue to operate the Zantel brand, while delivering cash flow growth by leveraging technical and operational efficiencies. The company plans to roll out 4G coverage and access more bandwidth capacity via the undersea fibre optic cable EASSy.

Millicom has arranged with a leading international bank, the provision of a USD 100 million 5-year credit facility for Zantel. The Government of Zanzibar will continue to own the remaining 15 percent of the shares in Zantel. The transaction remains subject to regulatory approval by the Tanzanian Communications Regulatory Authority and the Fair Competition Commission.

Zantel is the leading mobile telecom operator on the islands of Zanzibar with 2014 gross revenues of USD 82 million and 1.7 million subscribers across Zanzibar and mainland Tanzania. It operates 2G and 3G services over 545 network sites, with 57MHz of spectrum1 and has ownership rights to undersea fibre optic cable capacity. Zantel has an approximate 5 percent share of the Tanzania mobile market.

Yemen: Saudia inatumia silaha zilizopigwa matukufu

Wizara ya Afya ya Yemen imetangaza kuwa Saudi Arabia imetumia silaha zilizopigwa marufuku kimataifa dhidi ya wananchi wa Yemen katika mashambulio yake ya kijeshi katika nchi hiyo ya Kiarabu. Tamim Shami Msemaji wa Wizara ya Afya ya Yemen ameeleza kuwa baadhi ya watu waliojeruhiwa katika mashambulizi ya Saudia wana dalili zinazoashiria kwamba wameathiriwa na silaha ziliopigwa marufuku zilizodondoshwa na ndege za Saudi Arabia katika mashambulizi yake katika mji mkuu wa Yemen Sana’a yaliyoanza Machi 26 mwaka huu pasina kuidhinishwa na Umoja wa Mataifa.  
Msemaji wa Wizara ya Afya ya Yemen ameongeza kuwa nchi hiyo inasumbuliwa na hali inayozidi kuwa mbaya ya kibinadamu kutokana na kuwepo uhaba wa suhula za tiba. Amesema watu zaidi ya 5,000 wanaugua homa ya dengue na malaria. 

Misri yafungua tena kivuko cha mpakani cha Rafah

Serikali ya Misri leo imekifungua tena kivuko cha Rafah kilichoko kwenye mpaka wa pamoja wa nchi hiyo na Ukanda wa Gaza ili kuwaruhusu Wapalestina kuingia na kutoka katika eneo hilo, ikiwa ni mara ya kwanza katika kipindi cha miezi mitatu, katika kile kinachoonekana kama ishara ya kupungua mvutano uliokuwepo kati ya Cairo na Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS iliyoshika hatamu za eneo la Gaza. Ukanda wa Gaza umewekewa mzingiro na utawala wa Kizayuni wa Israel kwa zaidi ya mwaka wa saba sasa, na serikali ya Misri imekuwa ikikifunga kivuko cha Rafah kwa muda mwingi tangu Rais Mohammad Morsi aliyekuwa na uhusiano wa karibu na Hamas alipoondolewa madarakani mwaka 2013. Wiki mbili zilizopita Cairo ilikifungua kituo cha Rafah kwa muda wa siku tatu kuruhusu safari za upande mmoja tu kwa Wapalestina waliokuwa wamekwama nje ya Ukanda wa Gaza kuweza kurejea makwao katika eneo hilo. Lakini hatua ya leo ya kuruhusu kuingia na kutoka Gaza kupitia kivuko cha Rafah inaonekana kama ishara ya kuboreka uhusiano wa Misri na Hamas baada ya msuguano na mvutano mkali uliokuwepo kwa muda wa miaka miwili. Serikali ya Cairo imeituhumu Hamas kuwa inayaunga mkono makundi ya wanamgambo wenye silaha yanayopambana na serikali ya Misri katika Rasi ya Sinai, tuhuma ambazo Hamas imezikadhibisha. Maafisa katika mpaka wa Misri na Palestina inayokaliwa kwa mabavu wamesema kivuko cha Rafah kitaendelea kuwa wazi kwa muda wa siku tatu, huku baadhi ya duru za Palestina zikieleza kwamba muda huo unaweza kuongezwa; hata hivyo hakuna kauli yoyote iliyotolewa na maafisa wa Misri kuthibitisha suala hilo…

Iran yatoa radiamali kupinga taarifa ya PGCC

Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amepinga taarifa ya hivi karibuni ya Baraza la Ushirikiano la Ghuba ya Uajemi kuhusu visiwa vitatu vya Iran. Bi Marzieh Afkham amejibu matamshi hayo ya Baraza la Ushirikiano la Ghuba ya Uajemi kwa kusema kuwa: Kukaririwa madai yasiyo na msingi hakujakuwa na athari kwa uhakika wa kihistoria. Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema visiwa vya Bumusa, Tomb Kubwa na Ndogo ni sehemu ya ardhi ya Iran isiyoweza kutenganishwa. Afkham ameongeza kuwa:  Iran inatoa kipaumbele katika siasa zake kwa suala la kuwa na uhusiano mwema na majirani zake, uhusiano ambao umejengeka kwa kutoingilia masuala ya nchi nyingine na kuheshimiana pande mbili na haina kizuizi chochote katika kustawisha na kupanua mahusiano ya kirafiki. Bi Afkham amesema Iran inakaribisha kuwepo maelewano na ushirikiano mkubwa wa pande zote na majirani zake

Bush amtaka Obama atume wanajeshi wa US Iraq

Rais wa zamani wa Marekani George W. Bush amemkosoa Rais wa nchi hiyo Barack Obama kutokana na stratijia anayotumia katika vita dhidi ya kundi la kigaidi na kitakfiri la Daesh (ISIL) na kusema kuwa Washington inapaswa itume wanajeshi wake nchini Iraq. Bush amesema msimamo wake ni kwamba kuna haja ya kutuma vikosi vya nchi kavu nchini Iraq. Bush amedai kuwa serikali yake iliushinda mtandao wa kigaidi wa al-Qaeda wakati ilipotuma askari wa ziada nchini Iraq. Barack Obama amekuwa akilaumiwa vikali kwa kushindwa kulisambaratisha kundi la kigaidi na kitakfiri la Daesh katika nchi za Iraq na Syria. Mapema wiki hii Obama alikiambia kikao cha nchi tajiri zinazounda kundi la G7 kilichofanyika nchini Ujerumani kwamba hawajawa na stratijia iliyokamilika dhidi ya Daesh. Tangu mwaka uliopita serikali ya Washington imekuwa ikiongoza operesheni za mashambulio ya anga dhidi ya ngome za kundi la kigaidi na kitakfiri la Daesh lakini mashambulio hayo hayajapata mafanikio yoyote. Siku ya Jumatano iliyopita, msemaji wa Ikulu ya Marekani Josh Earnest alisema Rais Obama ametoa amri ya kutumwa askari 450 wa ziada nchini Iraq kwa ajili ya kutoa ushauri kwa vikosi vya nchi hiyo kutokana na ombi la Waziri Mkuu Haidar al-Abadi. Askari hao wataifanya idadi ya askari wote wa Marekani walioko nchini Iraq ifikie 3,550. Kwa mujibu wa Wizara ya Ulinzi ya Marekani Pentagon, hadi sasa nchi hiyo imeshatumia zaidi ya dola bilioni 2.7 katika operesheni za kijeshi dhidi ya Daesh katika nchi za Iraq na Syria ambazo ni wastani wa zaidi ya dola milioni tisa kwa siku…/

Wednesday, 10 June 2015

Zanzibar and Comoro signed MOU for business and trade development among the two countries



THE Comorian Union Chambers o Commerce, Industry and Agriculture UCCIA and their counterpart from Zanzibar National Chamber of Commerce, Industry and Agriculture ZNCCIA put hands to gather as a symbol of unity after they have signed MoU that aiming to foster business and trade development among the two countries during the ceremony in Moron. The only lady seen in the picture is Mtwara Regional Commissioner, Halima Dendego. President of Comorian Union Chambers o Commerce, Industry and...

RAIS WA ZANZIBAR DR. SHEIN AONGEA NA WATANZANIA WANAOISHI UJERUMANI MJINI WUERZBURG



Mwenyekiti wa Umoja wa Tanzania Ujerumani Bw. Mfundo Peter Mfundo (aliyesimama) akimkaribisha Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein.Baadhi ya Watanzania waishio Ujerumani katika picha ya pamoja na Rais Dr.Shein.Balozi wa Tanzania nchi Ujerumani Bw.Philip Marmo akimwagia sifa za Watanzania waishio nchini Ujerumani kwa Rais Dr.Shein.Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein akiwa na Watanzania waishio Ujerumani.
WUERZBURG,...

Saturday, 6 June 2015

Saudia yaendeleza jinai zake nchini Yemen

Nyumba za raia zilizoharibiwa katika hujuma ya Saudia Yemen Nyumba za raia zilizoharibiwa katika hujuma ya Saudia Yemen
Saudi Arabia imeendeleza jinai zake za kivita nchini Yemen huku makumi ya raia wasio na hatia wakiuawa katika hujuma za leo.
Kwa mujibu wa shirika rasmi la habari la Yemen, Saba, katika hujuma ya ndege za kivita za Saudi Arabia leo Ijumaa katika maeneo mbali mbali ya Yemen hasa mikoa ya Sa'ada, Hajja na Aden, raia wasiopingua 40 wameuawa na wengine kadhaa kujeruhiwa.  Ndege za kivita za Saudi Arabia pia zimedondosha mabomu katika hospitali katika mji wa Dhamar mbali na kuhujumu pia chuo kikuu mjini humo.
Huku hayo yakijiri makumi ya maelfu ya watu wameandamana katika mji mkuu wa Yemen, Sana'a kupinga na kulaani hujuma ya kijeshi ya Saudi Arabia dhidi ya nchi yao.
Kwa mujibu wa ripoti ya hivi karibuni ya Taasisi ya Uhuru ya Yemen, tangu yalipoanza mashambulio ya kivamizi ya Saudia dhidi ya nchi hiyo Machi 26 mwaka huu ambayo yamefanywa bila ya idhini ya Umoja wa Mataifa, hadi sasa watu wasiopungua 4,000 wameshauawa na wengine 7,000 kujeruhiwa.  Aghalabu ya wahanga wa hujuma hizo zinazoongozwa na Saudia ni watoto, wanawake na raia wa kawaida wasio na hatia

Mikutano ya siri ya Saudia na Israel kuhusu Iran

Anwar Majed Eshki (kushoto) kutoka Saudia na Dore Gold wa Israel Anwar Majed Eshki (kushoto) kutoka Saudia na Dore Gold wa Israel
Ripoti imefichuka kuhusu mikutano kadhaa ya siri baina ya wawakilishi wa Saudi Arabia na Israel kwa lengo la kujadili misimamo yao kuhusu Iran.
Kwa mujibu wa tovuti ya Bloomberg, mikutano hiyo imefanyika mara tano katika kipindi cha miezi 17 iliyopita ambapo maafisa hao wa Saudia na utawala haramu wa Israel wamekutana nyakati mbali mbali huko India, Italia na Jamhuri ya Czech.
Tovuti hiyo imenukulu jenerali mstaafu katika jeshi la Israel aliyeshiriki katika moja ya vikao hivyo akisema, "Tuligundua kuwa tunakabiliana na matatizo na changamoto za pamoja na pia baadhi ya majibu ya pamoja." Aidha siku ya Alkhamisi maafisa mashuhuri wa zamani wa Saudia na Israel walikutana katika taasisi za Council on Foreign Relations huko Washington. Kikao hicho kilihudhuriwa na Anwar Majed Eshki, mshauri wa zamani wa serikali ya Saudia, na Dore Gold balozi wa zamani wa Israel aliye karibu na Waziri Mkuu wa Utawala wa Kizayuni Benjamin Netanyahu. Israel na Saudia zote kwa pamoja zinapinga kile zinachosema ni kuenea ushawishi wa Iran katika eneo. Aidha pande mbili hizo zimetangaza wazi kupinga mapatano ya nyuklia baina ya Iran na madola sita makubwa duniani. Hivi karibuni pia gazeti moja la Uingereza lilisema Israel imetangaza kuwa tayari kuipa Saudia makombora katika vita vyake dhidi ya watu wa Yemen

'Umaanawi wa mfumo wa Kiislamu Iran ni wa kipekee'

Ayatullah Mohammad Imami Kashani Ayatullah Mohammad Imami Kashani
Khatibu wa Sala ya Ijumaa mjini Tehran amesema mfumo wa Kiislamu wa Iran ni wa kipekee duniani kutokana na umaanawi wake. Ayatullah Mohammad Imami Kashani, khatibu wa muda wa sala ya Ijumaa wiki hii Tehran ameashiria umuhimu na nafasi ya mfumo wa Kiislamu wa Iran na tafauti yake na mifumo mingine duniani na kusema: "Sira ya kivitendo ya Imam Khomeini MA, muasisi wa Jamhuri ya Kiislamu ni yenye thamani kubwa sana ambayo inapaswa kuzingatiwa na  jamii hasa kizazi cha vijana." Ayatullah Imami Kashani aidha ameashiria namna Imam Khomeini MA alivyolipatia umuhimu suala la umoja wa ulimwengu wa Kiislamu na kusema: "Umoja wa Waislamu, uchumi, maisha bora ya wananchi, na kumfahamu adui ni kati ya nukta muhimu katika sira ya kivitendo ya Imam." Ameongeza kuwa sira ya kivitendo ya Imam Khomeini MA haiwezi kamwe kupotoshwa. Khatibu wa Sala ya Ijumaa ameongeza kuwa: 'Baada ya kuaga dunia Imam Khomeini MA, uwepo wa Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Khamenei, ni neema kubwa kwa Jamhuri ya Kiislamu. Wilaya au uongozi wake ni muhimu sana kwa mfumo na jamii a Kiislamu kwa sababu anafuata ile ile njia ya Imam Khomeini MA."  Ayatullah Kashani ameashiria nafasi ya 'Faqihi Mtawala' au Wilayat Faqih katika mfumo wa Kiislamu na kusema wale ambao wanatilia shaka utawala huo ni maadui wa mfumo wa Kiislamu.  Khatibu wa Muda wa Sala ya Ijumaa sambamba na kuelezea matumaini yake kuwa kadhia ya nyuklia itatatuliwa sambamba na kuhifadhiwa haki za taifa la Iran, ametoa wito kwa timu ya Iran katika mazungumzo ya nyuklia kulinda haki za taifa hili

Kenya yawaonya wafanyamagendo ya pembe za ndovu

Rais Uhuru Kenyatta Rais Uhuru Kenyatta
Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya ametahadharisha maafisa wa serikali yake wanaojihusisha na biashara haramu ya pembe za ndovu akisema watakamatwa na kufikishwa mbele ya vyombo vya sheria. Akizungumza mapema leo kwenye mkutano wa wawekezaji mjini Nairobi, Rais Kenyatta ameagiza maafisa wa usalama kuchunguza kesi inayohusiana na kukamatwa kwa shehena kubwa ya pembe za ndovu huko Thailand mwezi Aprili ambayo inaaminika kutoka Kenya na kuwafikisha wahusika wote mbele ya vyombo vya sheria. Pia Rais wa Kenya ameonya wawekezaji na maafisa wa idara za serikali wanaojihusisha na uingizaji wa bidhaa bandia nchini akisema chuma chao ki motoni. Kiongozi huyo amesema bidhaa bandia zinazoingizwa Kenya zinachangia soko la ndani kuporomoka na hivyo kuwafanya vijana wengi kukosa nafasi za ajira. Pia amesema jmbo hilo linahatarisha usalama wa taifa kwani bidhaa ghushi zinazoingizwa hazikaguliwi na hivyo kuna uwezekano wa kuingizwa hata silaha kupitia njia hizo.
Maafisa kadhaa wa idara ya forodha pamoja na wale wa mamlaka ya ukusanyaji ushuru wamekamatwa na kufikishwa kortini kuhusiana na biashara haramu ya meno ya tembo

Marekani yapinga Kagame kugombea muhula wa 3

Paul Kagame Paul Kagame
Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani imesema haiungi mkono rais wa Rwanda, Paul Kagame kugombea tena muhula wa tatu kwenye uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika mwaka 2017. Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani anayehusika na masula ya Afrika amewambia waandishi wa habari mjini Washington kuwa, Rwanda inahitaji kuwa na taasisi zenye nguvu zitakazosimamia uimarishwaji wa demokrasia na wala haihitaji mtu mwenye nguvu kufanya kazi hiyo.
Siku chache zilizopita, wabunge wa Rwanda walifichua kwamba, mamilioni ya Wanyarwanda wamemuomba Rais Paul Kagame kuendelea kuwaongoza hata baada ya 2017. Kwa msingi huo, wabunge hao wamesema watachunguza kwa makini maombi hayo ya wananchi na iwapo yatakuwa na uzito, wataanza mchakato wa kubadilisha katiba ili kuondoa kifungu kinachoweka kikomo kwa muhula wa rais kuongoza. Kwa sasa katiba ya Rwanda inasema rais anayechaguliwa hawezi kuzidisha zaidi ya mihula miwili madarakani

Waliokufa katika mlipuko Ghana wafika hadi 175

Habari kutoka Ghana zinasema kuwa, idadi ya watu waliofariki dunia kufuatia moto uliotokea katika kituo kimoja cha mafuta katika mji mkuu Accra imepanda na kufikia 175. Duru za hospitali zinasema watu wengi waliokimbizwa kwenye vituo vya matibabu wakiwa na majeraha mabaya ya moto wamefariki dunia kati ya jana usiku na leo mchana. Mlipuko huo ulitokea siku ya Jumatano wakati mamia ya watu walipokuwa wamejihifadhi katika kituo cha mafuta kutokana na mvua kubwa zilizokuwa zikinyesha. Tarayi Ghana imetangaza siku tatu za maombolezo ya kitaifa kufuatia vifo hivyo. Rais John Dramani Mahama ambaye ametemelea eneo la mkasa huo amesema taifa limetikiswa na idadi kubwa ya watu waliopoteza maisha kwenye mlipuko huo.
Mvua za masika zinazoendelea kunyesha huko Ghana zimesababisha nyumba nyingi kuharibika na hivyo kuwaacha watu wengi bila makao. Wizara ya Afya ya nchi hiyo imetahadharisha