Unordered List


Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Wednesday, 19 November 2014

Wabunge waomba muongozo wa spika kuweka muda kujadili taarifa ya PAC kuhusu kashfa ya shilingi Bilioni 200 ya akaunti ya ESCROW.


Wabunge waomba muongozo wa spika kuweka muda kujadili taarifa ya PAC kuhusu kashfa ya shilingi Bilioni 200 ya akaunti ya ESCROW.
Baadhi ya wabunge wameomba mwongozo wa spika unaotaka kamati ya uongozi kweka muda wa kusitisha kujadili taarifa ya kamati ya PAC kuhusu sakata la wizi wa fedha katika akaunti Tegeta ESCROW bada ya kuona utaratibu uliopo unatoa muda mchache wa kujadili  hivyo kufunya uhuru wa wabunge kujadilisha taarifa inayowasilishwa na kamati.
Akiomba mwongozo kwa naibu spika, mbunge wa mtera Mhe.Livingstone Lusinde ametaka kamati ya uoungozi kuongeza muda wa kujadili tuhuma zinazojitokeza na hasa zinagusa baadhi ya mawaziri na wabunge wenyewe ambao wanalalamikiwa.
 
Katika hatua nyingine kamati ya kudumu ya bunge ya uchumi,viwanda na biashara ikitoa maoni kuhusu mswada wa marekebisho ya sheria ya ubia baina ya sekta ya umma na sekta binafsi wa mwaka 2014 imesema changamoto zinazoikabili serikali ni kutokuwepo kwa sera zinazowalinda wazawa kushiriki katika uwekezaji nchini. 
 
Wakichangia muswada wa marekebisho ya sheria ya ubia na bina ya sekta ya umma na sekta binafsi,baadhi ya wabunge wamehoji serikali inampango gani wa kuwawezesha wawekaji wa ndani kama ambavyo nchi nyingine zinazoendelea na zisizoendela zinafanya katika kuwajengea uwezo watu wake.
 
Awali akiwasilisha muswada huo waziri wa nchi ofisi ya waziri mkuu uwekezaji na uwezeshaji, Mhe.Mary Nagu amesema mapendekeza hayo yanalenga kuongeza utekelezaji wa miradi ya ubia pamoja na mazingira yatakayowezesha sekta binafsi kushiriki kikamilifu katika kuwekeza katika miradi ya kiuchumi na kijamii.

No comments:

Post a Comment