Unordered List


Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Wednesday, 19 November 2014

Ukawa yabaini Njama za Kuondoa Mjadala juu Kashfa ya fedha Bilioni 321 za Akaunti Ya Tegeta ESCROW kwa Kutumia Mgongo Wa Mahakama.

Ukawa yabaini Njama za Kuondoa Mjadala juu Kashfa ya fedha Bilioni 321 za Akaunti Ya Tegeta ESCROW kwa Kutumia Mgongo Wa Mahakama.
Umoja wa katiba ya wananchi-Ukawa imebaini kuwepo kwa njama za kutaka kuondoa mjadala wa wizi wa zaidi ya Bilioni 321 fedha zilizokuwa katika akaunti ya tegeta ESCROW Bungeni kwa kutumia chombo cha mahakama.
Akizungumza na waandishi wa habari,mwanasheria wa ukawa Mhe.Tundu Lissu amesema ipo taarifa ya barua kutoka mahakamani inazodai sakata la ESCROW liko mahakamani hivyo halipaswi kujadiliwa Bungeni,na kusisitiza hakuna utaratibu wowote mahakama unaoipa mamlaka ya kulieleleza Bunge jambo la kufanya.
 
kwa upande wake mwenyekiti  mwenza wa ukawa Mhe. James Mbatia amesema Bunge linahitaji muda wa kutosha kuhakikisha kashfa hiyo inajadiliwa kwa upana na baada ya uchunguzi wa Ripoti ya PAC kuonyesha Bunge watakaotuhumiwa  swala la kisiasa,kisheria wawajibishwe. 
 
Hivi karibu,naibu spika wa bunge alikabidhi Ripoti ya mdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali kuhusu wizi wa zaidi ya shilingi Bilioni 321 fedha zilizokuwa katika akaunti ya Tegeta ESCROW ambao inadaiwa kuhusisha baadhi ya viongozi mbalimbali wa serikalini.

No comments:

Post a Comment