Unordered List


Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Thursday, 27 November 2014

Hii ndiyo sababu ya kufunguliwa escrow



Dar es Salaam. Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), Zitto Kabwe ameanika chanzo cha kufunguliwa kwa Akaunti ya Tegeta Escrow kuwa ni mgogoro ulioibuka kati ya Tanesco na IPTL.
Akitoa ripoti ya uchunguzi wa akaunti ambayo Sh306 bilioni zilichotwa na IPTL, Zitto alisema ilianzishwa chini ya wanahisa wawili; Kampuni ya Mechmar Malaysia Berhad iliyosajiliwa Malaysia ambayo ilikuwa inamiliki hisa saba sawa na asilimia 70 katika IPTL na Kampuni ya VIP Engineering and Marketing iliyosajiliwa nchini ikiwa na hisa tatu sawa na asilimia 30 ya hisa zote.
Alisema mwaka 1995, Serikali kupitia Tanesco iliingia Mkataba wa miaka 20 na IPTL kwa ajili ya kuzalisha na kuuziana umeme wa megawati 100 japokuwa makubaliano ya awali (MoU) yalionyesha kuwa mkataba ungekuwa wa miaka 15.
“Hata hivyo, Tanesco ilibaini kwamba gharama za ujenzi wa mtambo wa kuzalisha umeme ambazo IPTL iliwasilisha kwake zilikuwa kubwa tofauti na makubaliano ya kwenye mkataba,” alisema. Alisema IPTL ilikuwa imefunga injini zenye msukumo wa kati (medium speed) zenye gharama ndogo na uwezo mdogo badala ya injini za msukumo mdogo (low speed) zenye nguvu kubwa na bei kubwa.
“Wakati huohuo, IPTL waliendelea kutoza kiasi kikubwa cha fedha kinacholingana na gharama ya ufungaji wa mtambo wenye msukumo mdogo (low speed). Katika utekelezaji wa Mkataba IPTL walitakiwa kufunga jenereta tano zenye uwezo wa kuzalisha megawati 20 kila moja lakini badala yake walifunga jenereta 10 zenye uwezo wa kuzalisha megawati 10 kila moja, jambo ambalo lilikuwa ni kinyume na makubaliano ya mkataba,” alisema.
Kutokana na IPTL kukiuka mkataba, alisema mwaka 1998 Tanesco ilifungua kesi katika Baraza la Kimataifa la Usuluhishi wa Migogoro ya Uwekezaji (ICSID) kupinga ukiukwaji huo na hukumu iliyotolewa na ICSID; IPTL iliagizwa kupunguza gharama za uwekezaji kutoka Dola 163.531 milioni hadi 127.201 milioni kwa mwezi. Alisema ujenzi wa mitambo ulikamilika mwaka 1997, uzalishaji na uuzaji wa umeme ulianza mwaka 2002.
Alisema kuanzia mwaka 2002, gharama za uwekezaji kutokana na uwepo wa mtambo wa kuzalisha umeme, zilianza kulipwa na Tanesco kwa IPTL, huku gharama za uendeshaji zikiendelea kulipwa kwa muda wote ambao mkataba unaendelea bila ya kujali kama mtambo unazalisha umeme au hauzalishi.
“Gharama zilikoma kulipwa moja kwa moja kwa IPTL mwaka 2007 baada ya Tanesco kubaini kuwa IPTL inakokotoa gharama hizo kwa msingi wa Dola 38.16 milioni (ambayo ni sehemu ya mkopo wa Dola 105 milioni uliochukuliwa na wanahisa kutoka umoja wa benki za Malaysia, ambao baadaye ulinunuliwa na Benki ya Standard Chartered ya Hong Kong, badala ya mtaji wa uwekezaji wa Sh50,000 uliosajiliwa Brela.)
“Hali hii ilifanya tozo ya gharama za uendeshaji kuwa kubwa. Endapo ungetumika mtaji wa uwekezaji wa Sh50,000 katika kukokotoa gharama za uendeshaji, Tanesco ingekuwa inalipa tozo ndogo kuliko ilivyo sasa,” alisema.
Alisema hiyo ndiyo ilikuwa sababu ya mwaka 2004, Tanesco kufungua kesi ya pili kupinga kiasi kikubwa cha tozo ya gharama za uendeshaji na kwamba uamuzi wa Baraza ilikuwa ni wanahisa waketi na mteja wao (Tanesco) na kukubaliana kuhusu kanuni ya ukokotoaji wa tozo hiyo.
“Mpaka sasa tunapowasilisha taarifa hii bungeni, uamuzi wa ICSID-2 kwamba IPTL ikae na Tanesco kwa ajili ya kukokotoa upya gharama za uendeshaji haujatekelezwa, hivyo Tanesco wanaendelea kulipa Dola za Marekani 2.6 milioni (Sh4.5 bilioni kwa mwezi),” alisema.
Escrow kufunguliwa
Zitto alisema kwa mujibu wa taarifa ya CAG, imebainika kuwa chanzo cha mgogoro kati ya Tanesco na IPTL ambacho ndicho kilichosababisha kufunguliwa kwa Akaunti ya Tegeta Escrow ni taarifa ziliyoifikia Bodi ya Wakurugenzi ya Tanesco.
Alisema katika taarifa hiyo, pamoja na mambo mengine ilifahamishwa na mmoja wa wanahisa wa IPTL, Kampuni ya VIP Engineering, kuwa kuna viashiria kuwa Tanesco wanailipa IPTL gharama kubwa za uendeshaji.

Tuesday, 25 November 2014

Utapeli kwa jina la Mungu

Somali Islamists execute 28 non‑Muslims on Kenya bus

Somalia's Shebab Islamists on Saturday seized a bus in Kenya, executing 28 non-Muslim passengers in what they said was revenge for police raids on mosques in the troubled port of Mombasa.
"I can confirm... that 28 innocent travellers were brutally executed by the Shebab," regional police chief Noah Mwavinda told AFP.
The bus, which was headed for the capital Nairobi, was ambushed shortly after departing from Mandera, a town lying on the border with Somalia in Kenya's northeasternmost corner.
The around 60 passengers on board were ordered off and the travellers separated by the gunmen into Muslims and non-Muslims.
The militants then had the non-Muslims reboard the bus and tried to drive off with them, but the vehicle got stuck.
"So they executed their prisoners" before escaping back into Somalia, Mwavinda said.
Kenya's Red Cross confirmed the death toll in a tweet after its team arrived at the scene.
A Shebab spokesman said the deadly attack was in revenge for raids early this week on four Mombasa mosques that added to the simmering tensions in the city.
"The Mujahedeen successfully carried out an operation near Mandera early this morning, which resulted in the perishing of 28 crusaders, as a revenge for the crimes committed by the Kenyan crusaders against our Muslim brethren in Mombasa," Ali Mohamud Rage said in a statement sent to AFP.
Police this week closed the four mosques in Mombasa, a largely Muslim city unlike much of Kenya where Christians make up 80 percent of the population, on the grounds they had come under the influence of hardliners.
- 'Rats in a granary' -
Britain and the United States condemned the attack, pledging to help Kenya combat such actions.
"The United States stands with our Kenyan partners in the effort to counter the threat of terrorism," US National Security Council spokeswoman Bernadette Meehan said in a statement, deploring the "horrific attack".
In London, Hugo Swire, minister of state for the Foreign and Commonwealth Office, said "the UK stands by the Kenyan government in its fight against terrorism."
A 25-year-old passenger on the bus, who asked to be identified only as Ibrahim, told AFP that the vehicle came under fire several times after leaving Mandera, leaving one passenger dead.
The driver tried to escape but was finally forced to stop by the group of around 70 assailants, he said.
"After the bus came to an abrupt halt due to the showering bullets... all the passengers were put into two groups, one for those they thought were Muslim, and those they thought were not," he said.
The attackers, who identified themselves as members of the Shebab, read verses from the Koran to the Muslims, urging them to combat the Kenyan authorities.
Ibrahim said they were then ordered to walk to a nearby village.
He said he witnessed the execution of two non-Muslim passengers, who were shot in the head.
Ibrahim quoted one of the attackers as saying: "We must fight those persecuting Muslims and closing our places of worship like rats found in a granary".
- Shebab a threat despite strikes -
Kenya has suffered a series of attacks since invading Somalia in 2011 to attack the Shebab, later joining an African Union force battling the Islamists.
Mandera County Assembly member Abdullahi Abdirahman said local leaders "have pleaded with the government to provide security, but they have turned deaf ears."
"Today we are experiencing avoidable massacre," he said.
The Shebab carried out the September 2013 attack on Nairobi's Westgate shopping mall, killing at least 67 people, as a warning to Kenya to pull its troops out of southern Somalia.
During the Westgate attack, some of the victims were killed after the gunmen weeded out non-Muslims for execution by demanding they recite the Shahada, the Muslim profession of faith.
The Shebab has lost a series of key towns and ports to the AU force and Somalian government army, heralded as advances that would stem the militants' multi-million dollar business trading charcoal to Gulf countries.
But in a recent report, UN investigators warned that the air and drone strikes on the militia have done little to damage it in the long term and that the insurgents continue to pose a serious regional threat.
Indeed, pressure on the fighters has forced them to "become more operationally audacious by placing greater emphasis on exporting its violence beyond the borders of Somalia" and across the Horn of Africa, said an October report by the UN Monitoring Group on Somalia and Eritrea

Serikali imewekeza katika siasa, imesahau wakulima

Serikali imewekeza katika siasa, imesahau wakulima

 
Hata hivyo, wakulima wamekwazwa na kodi nyingi wanazotozwa kwa kila gunia inapotokea wakauza sehemu ya mahindi yao yaliyolundikana. Malipo hayo ni kama kodi ya halmashauri, gharama za kuhifadhi mahindi ghalani, ubebaji wakati wa kushusha mahindi kituoni, kuchekecha mahindi, kuondoa uchafu na kupeleka kwenye mizani. 
Kwa ufupi
Siyo siri kuwa, iwapo fedha inazotumia katika mambo ya kisiasa zingeelekezwa kwenye kilimo, wakulima wangejikomboa kiuchumi.
Zipo dalili nyingi zinazoonyesha kwamba kuna uwezekano mkubwa nchi yetu ikakumbwa na janga kubwa la njaa mwakani. Kinachoendelea hivi sasa ni wakulima katika mikoa inayolima mazao ya chakula kwa wingi kukata tamaa kutokana na mazao yao kukosa soko, huku wakulima hao wakijikuta katika ufukara wa kutisha kutokana na kuwekeza fedha zao katika kilimo cha mazao hayo, lakini Serikali imeshindwa kuwatafutia masoko.
Hapa hatuzungumzii mazao ya biashara kama korosho, tumbaku, kahawa na pamba ambayo kwa muda mrefu sasa yamegeuka kuwa laana kwa wakulima kutokana na viongozi wa vyama vya ushirika nchi nzima kuvigeuza vyama hivyo kama mitaji binafsi ya kujitajirisha wakishirikiana na baadhi ya viongozi serikalini.
Kwa miongo minne sasa wakulima hao hawana sauti wala mtetezi. Serikali ingetarajiwa kuvikwamua vyama hivyo, ambavyo vilianzishwa na wakulima wenyewe na kuwa nguzo yao kubwa kiuchumi. Hata hivyo, hakuna asiyejua kwamba Serikali kwa kuogopa nguvu ya vyama hivyo, iliingilia kati na kuvisambaratisha kwa kupandikiza uongozi uliowekwa mfukoni na wanasiasa.
Hapa tunazungumzia wakulima wa mazao ya chakula, hasa mahindi yanayolimwa kwa wingi katika mikoa ya Mbeya, Rukwa, Katavi, Ruvuma, Iringa na Morogoro inayojulikana kama ‘Kapu la Chakula’. Hivi sasa wakulima wa zao hilo wamekata tamaa kutokana na kukosa soko la zao hilo, hivyo hawaoni tena sababu ya kuwekeza katika kilimo hicho kutokana na hasara waliyoipata msimu uliopita, ambao walikopa fedha kuandaa mashamba na kununua pembejeo na kufanikiwa kuvuna kiasi kikubwa cha mahindi. Wakulima walihamasika kutokana na Rais Jakaya Kikwete kutangaza bei mpya ya mahindi kutoka Sh350 hadi Sh500 alipokuwa katika ziara ya mkoani Ruvuma mwaka uliopita.
Matokeo yake ni kwamba mahindi yanaozea katika makazi ya watu, maghala ya vyama vya ushirika, Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NRFA) na wafanyabiashara binafsi. Wakulima wamebaki wakiwa midomo wazi, wakisubiri kuona miujiza ya mahindi yao kupata soko ili wajikwamue katika ufukara na umaskini uliopitiliza. Takwimu zinaonyesha kwamba mikoa hiyo imezalisha tani milioni 16 za mahindi, huku Mkoa wa Rukwa pekee ukizalisha tani milioni nne.
Hata hivyo, wakulima wamekwazwa na kodi nyingi wanazotozwa kwa kila gunia inapotokea wakauza sehemu ya mahindi yao yaliyolundikana. Malipo hayo ni kama kodi ya halmashauri, gharama za kuhifadhi mahindi ghalani, ubebaji wakati wa kushusha mahindi kituoni, kuchekecha mahindi, kuondoa uchafu na kupeleka kwenye mizani.
Kutokana na umuhimu wa sekta ya kilimo ambayo inatoa ajira kwa zaidi ya asilimia 80 ya wananchi, tungetarajia Serikali iwekeze nguvu na rasilimali zake kwenye kilimo. Mipango ya Kilimo Kwanza na Matokeo Makubwa Sasa imeonekana kuwa ni nadharia zaidi kuliko utekelezaji. Ni kutokana na hali hiyo tunaishauri Serikali iwekeze kwa wakulima badala ya kuwekeza kwenye siasa. Siyo siri kuwa, iwapo fedha inazotumia katika mambo ya kisiasa zingeelekezwa kwenye kilimo, wakulima wangejikomboa kiuchumi.
Ni wakati wa Serikali sasa kufikiri nje ya kisanduku kwa kuwatafutia wakulima masoko ya uhakika kwa mazao yao, yakiwamo matunda kama nyanya, maembe, machungwa na nanasi yanayoozea mashambani kwa kukosa viwanda vya kusindika. Kipaumbele kiwekwe kwa wakulima na Serikali itambue kwamba wananchi hawawezi kupata shibe kutokana na siasa.

NASIBU ABDUL ALISHAFANYA VIBARUA ILI APATE FEDHA YA CHAKULA

NASIBU ABDUL ALISHAFANYA VIBARUA ILI APATE FEDHA YA CHAKULA

Na Mwandishi Wetu
ANAITWA Nasibu Abdul au maarufu kwa jina la Diamond. Alizaliwa saa kumi na moja jioni ya Oktoba 2, 1989 katika Hospitali ya Amana iliyopo Wilaya ya Ilala jijini Dar es Salaam. Wazazi wake walimpa jina la Nasibu wakiamini ni la bahati.
Mkali wa Bongo fleva, Nasibu Abdul au maarufu kwa jina la Diamond akipozi.
Diamond aliongea hivi karibuni na safu hii ya Mjue Huyu ambapo aliweka wazi mambo mengi ya maisha yake. Diamond akiwa hajapata ufahamu, yaani bado mdogo, wazazi wake walitengana kwa sababu ambazo bado hazijawa wazi na baba yake kumuacha na mama.
WAZAZI WATENGANA, DIAMOND AENDA KWA BIBI
Kufuatia hali hiyo, ilibidi mama yake ahamie kwa mama yake mzazi (bibi wa Diamond), Tandale Magharibi, Dar. Hapo ndipo yakawa makazi ya mama huyo na mwanaye.
Mnamo mwaka 1995, Diamond alianza  elimu ya awali katika Shule ya Chakula Bora iliyopo Tandale- Uzuri. Mwaka 1996 alianza elimu ya msingi katika Shule ya Msingi Tandale- Magharibi iliyopo jijini Dar es Salaam.
DALILI YA KUWA MWANAMUZIKI
Mwaka 2000, Diamond akiwa darasa la tano alianza kupenda muziki, hivyo akawa anakopi baadhi ya nyimbo za wasanii waliokuwa wakihiti ndani na nje ya Bongo na kuimba yeye katika maeneo mbalimbali ya Jiji la Dar es Salaam. Kwa kuliona hilo, mama yake alianza kumnunulia kanda za albamu za wasanii tofauti hata kumwandikia baadhi ya nyimbo za wasanii hao ili mwanae aweze kuzishika na kuimba kirahisi.
ASOMA, APELEKWA KWENYE MATAMASHA
Diamond alizidi kuupenda muziki ikabidi mama yake awe anampeleka kwenye matamasha mbalimbali ili mwanae apate nafasi ya kuimba.
Baadhi ya ndugu walimjia juu mama huyo wakidai anamharibu mtoto badala ya kumuhimiza masomo anamwingiza kwenye muziki ambao walidhani haukuwa na faida yoyote.
MAISHA MAGUMU
“Kusema ukweli pamoja na yote hayo, hali ya maisha ilikuwa si nzuri kwa mama maana hakuwa na kazi ya maana wala vyanzo vikubwa vya fedha, hivyo  ilibidi atumie kiasi kidogo alichokipata kutoka kwenye kodi ya vyumba viwili alivyopewa na bibi ili kunisomesha,” alisema Diamond.
CHUMBA KIMOJA NA MAMA
Diamond aliendelea kusema kuwa, kutokana na kupangisha vyumba viwili ilibidi yeye na mama yake kuhamia kwenye chumba cha bibi yake na maisha yakaendelea humo.
AMALIZA SHULE YA MSINGI
Mwaka 2002, Diamond alimaliza masomo ya elimu ya msingi lakini ili aende sekondari, mama yake alimwambia aachane na habari ya muziki azingatie masomo aweze kupata elimu itakayomsaidia mbele ya safari katika maisha.
AFANYA MUZIKI KWA SIRI
Nyota huyo aliendelea kusema kuwa akiwa sekondari,  aliendelea kuimba muziki lakini kwa siri kubwa ili mama yake asijue.
Mwaka 2004, anasema alianza kuandika nyimbo zake mwenyewe kwa kuwa akili bado ilimwambia mafanikio yake yatapatikana huko.
AFANYA VIBARUA APATE PESA
Mwaka 2006, Diamond alimaliza elimu ya sekondari na kuanza kuimarisha ndoto yake ya kuwa mwanamuziki.
Alikuwa hana kazi ya kufanya nyumbani hivyo alianza kutafuta vibarua mbalimbali vya kumuwezesha kupata riziki ya siku. Miongoni mwa kazi hizo ni kuuza mitumba, kuweka mafuta kwenye magari (vituo vya mafuta), kupiga picha, kupigisha simu na kazi za kwenye viwanda mbalimbali.
Je, unajua nini kiliendelea? Usikose Jumanne ijayo.

ESCROW: WATAWALA WAWAJIBIKIE UDHAIFU, WEZI WATAFUATA

ESCROW: WATAWALA WAWAJIBIKIE UDHAIFU, WEZI WATAFUATA

Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe akikazia hoja.
YATOKANAYO na sakata la uchotwaji wa fedha kwenye akaunti maalum ya Tegeta Escrow iliyokuwa Benki Kuu ya Tanzania (BoT) ni mengi, lakini kubwa ni kuvuliwa nguo kwa utawala wa nchi. Akichangia bungeni hivi karibuni, Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe alisema mambo ya Escrow yalipaswa yafanyike kwenye nchi zisizokuwa na udhibiti wa dola, akitolea mfano Kongo na Somalia.
Katika hali ya kawaida yalikuwa ni maneno machache lakini mazito, sina hakika kama viongozi wa juu wa serikali walimwelewa alichomaanisha, pengine ndiyo maana sura zao hazikuonesha aibu juu ya kauli hiyo.
Lakini wenye kufikiri; matamshi hayo hayakuwa na sura njema kwa rais, waziri mkuu, mawaziri pamoja watendaji wa serikali vikiwemo vyombo vinavyosimamia usalama wa nchi.
Sarakasi za uchotwaji wa shilingi bilioni 306 katika akaunti ya Escrow zimepita kawaida na kusema kweli zinastaajabisha na kuogopesha mno.
Kwamba ‘wahuni’ wachache wanaweza kubuni uongo na kuielekeza BoT ambayo ni taasisi nyeti ya fedha za nchi itoe kiasi hicho kikubwa cha fedha bila vyombo vya usalama na watalawa kujua kinachoendelea, bila shaka alichokisema Zitto hakipingiki.
Kwa kukubaliana na hilo; nimeamua kuyapa makala haya kichwa cha habari hapo juu kwa mantiki kuwa hata kama viongozi wa ngazi za juu hawakuhusika moja kwa moja na sakata hilo bado hawawezi kukwepa udhaifu wa utawala wao.
Ikiwa vyombo vya usalama vilishindwa kubaini uchotwaji wa fedha nyingi kiasi hicho na kuwaacha watu wachache wakizifanyia mgawo ndani ya nchi wanayoiongoza, itakuwaje kwenye udhibiti wa fedha za miradi ya maendeleo kwenye halmashauri; watu si watajichotea watakavyo?
Ndiyo maana nimesema, viongozi ndani ya serikali wawajibikie kwanza udhaifu wao, watubu mbele ya umma kuwa wameshindwa kwa kiasi kikubwa kulinda mali za wananchi, baada ya hapo zamu ya wezi wa fedha za Escrow iwadie na wote waliohusika wapelekwe msalabani.
Kama njia hii ya uwajibikaji ikishindikana, udhaifu utaendelea kuwapa fursa wezi wa mali za wananchi na kila siku tutakuwa na wimbo mpya wa ufisadi, mara EPA, Richmond, Escrow na kadhalika zake.
Naandika makala haya katika sura hii si kama sielewi upande wa pili wa shilingi, la! Nimesikia hata Waziri Mkuu Mizengo Pinda naye anahusika katika sakata hili huku mtu anayeitwa ‘Bwana Mkubwa’ naye ametajwa kuujua mchezo.
Hili sikulipa kipaumbele sana kwa sababu watuhumiwa wanatumia nguvu kubwa sana kujinasua; wameulizwa mara kadhaa wamejitetea kuwa hawahusiki, lakini kutokuhusika kwa waziri mkuu kuna maana gani kama fedha nyingi kiasi hicho zimechotwa na yeye akiwa mwenye dhamana?
Kutohusika kwa rais wa nchi kuna maana gani kama bilioni 306 zimeibwa na wajanja wakati yeye akiwa na dhamana ya wananchi waliomchagua awaongoze na kuwalinda? Hapa ndipo niliposimamia, sitaki kuhukumu juu ya wizi nisiokuwa na ushahidi nao.
Narudia kusema; viongozi wa serikali, wameiba au hawajaiba wana jukumu la kuutubia udhaifu wao mbele ya wananchi kwa kushindwa kwao kujua njama za wizi mkubwa wa mali za umma.
Hili peke yake katika nchi zinazojali uwajibikaji, lilitosha kabisa kuwaondolea sifa baadhi ya watendaji na kuwapotezea sifa za uongozi bila kusubiri ushahidi wa kuhusika kwao moja kwa moja na wizi.
Nachochea tu!

GAPCO YAZINDUA KADI MAALUM ZA SAFARI ZITAKAZOWEZESHA DEREVA KUPATA UNAFUU WA BEI YA MAFUTA KATIKA VITUO VYOTE, TANZANIA

GAPCO YAZINDUA KADI MAALUM ZA SAFARI ZITAKAZOWEZESHA DEREVA KUPATA UNAFUU WA BEI YA MAFUTA KATIKA VITUO VYOTE, TANZANIA‏

 Rais wa Reliance Industries Limited ya Mumbai, Ashok Dhar akipongezana na Diwani wa Kata ya Kariakoo, Abdulkarim Masamaki (wa tatu kushoto) baada ya kuzindua kadi maalum za Safari za kampuni hiyo zitakazomwezesha dereva kupata huduma ya mafuta kutoka vituo vyote vya Gapco nchini kwa unafuu. Wengine (kustoka kushoto) ni Rais wa kampuni ya RIL ya Mumbai, Ashok Dhar, Diwani wa Kata ya Gerezani, Salum Bisarara, Ofisa Mtendaji Mkuu wa kundi la makampuni ya Gapco, Dk. Macharia Irungu na Mkurugenzi wa kituo cha Gapco, Barabara ya Nyerere, Muntazir Bharwani.
  Rais wa Reliance Industries Limited ya Mumbai, Ashok Dhar akikabidhi kadi maalum za Safari kwa Diwani wa Kata ya Gerezani, Salum Bisarara na Diwani wa Kata ya Kariakoo, Abdulkarim Masamaki baada ya kuzindua kadi hizo zitakazomwezesha dereva kupata huduma ya mafuta kwa unafuu katika hafla iliyofanyika Kituo cha Mafuta Gapco cha Kamata, Dar es Salaam jana. Wengine (kutoka kushoto) ni Rais wa kampuni ya RIL ya Mumbai, Ashok Dhar, Ofisa Mtendaji Mkuu wa kundi la makampuni ya Gapco, Dk. Macharia Irungu na maofisa wengine wa Gapco.
Rais wa Reliance Industries Limited ya Mumbai, Ashok akionesha kadi maalum za Safari za Gapco baada ya kuzinduliwa rasmi katika hafla iliyofanyika kituo cha mafuta cha Gapco Kamata, Dar es Salaam jana. Kadi hizo zitamwezesha dereva kuweza kupata huduma ya mafuta kwa unafuu kutoka vityo vyote vya Gapco Tanzania. Kutoka kushoto ni Ofisa Mwendeshaji Mkuu wa Gapco Tanzania, Vijay Nair, Diwani wa Kata ya Gerezani, Salum Bisarara, Diwani wa Kariakoo, Abdulkarim Masamaki (wa tatu kushoto), Meneja Miradi wa Gapco, Mohit Shirma, Ofisa Mtendaji Mkuu wa kundi la makampuni ya Gapco, Dk. Macharia Irungu na maofisa wengine wa Gapco.
 Meneja Uendeshaji wa Kadi za Gapco, Shital More akielezea matumizi ya kadi maalum za Safari kwa Diwani wa Kata ya Kariakoo, Abdulkarim Masamaki (katikati) baada ya kuzindua rasmi kadi hizo zitakazomwezesha dereva kupata huduma ya mafuta kwa unafuu katika vituo vyote vya Gapco nchini katika hafla iliyofanyika kituo cha Gapco Kamata, Dar es Salaam jana. Wengine (kutoka kushoto) ni Ofisa Mtendaji Mkuu wa kundi la makampuni ya Gapco, Dk. Macharia Irungu, Meneja Miradi wa Gapco Tanzania, Mohit Shirma, Rais wa kampuni ya Reliance Industries Limited ya Mumbai, Ashok Dhar na maofisa wengine wa Gapco.
Diwani wa Kata ya Kariakoo, Abdulkarim Masamaki (wa pili kulia) akifurahia jambo baada ya kuelekezwa matumizi ya kadi maalum za Safari Gapco na Meneja Miradi wa Gapco Tanzania, Mohit Shirma baada ya kuzindua kadi hizo, katika kituo cha mafuta cha Gapco Kamata, Dar es Salaam jana. Kushoto ni Ofisa Mtendaji Mkuu wa kundi la makampuni ya Gapco, Dk. Macharia Irungu na maofisa wengine wa Gapco.
 Ofisa Mtendaji Mkuu wa kundi la makampuni ya Gapco, Dk. Macharia Irungu akizungumza na wageni waalikwa wakati wa hafla ya uzinduzi wa kadi maalum za Safari zitakazomuwezesha dereva kupata unafuu wa mafuta kutoka katika vituo vyote vya Gapco, Dar es Salaam jana.
 Diwani wa Kata ya Kariakoo, Abdulkarim Masamaki akizungumza na wageni waalikwa wakati wa hafla ya uzinduzi wa kadi maalum za Safari zitakazomuwezesha dereva kupata unafuu wa mafuta kutoka katika vituo vyote vya Gapco, Dar es Salaam jana.
 
Kampuni inayoongoza kwa uuzaji wa bidhaa za mafuta nchini, imezindua programu aminifu kuwezesha wamiliki wa magari kujipatia pointi wakinunua mafuta ambazo zitawawezesha kupata ‘Mafuta Bure’ Kama faida.
Mpango huu utawanufaisha wakazi wa Dar es Salaam, kwa kuanzia na nchini kote mwakani.
Jerry Slaa, Maya wa Manispaa ya Ilala akizungumza katika sherehe ya uzinduzi iliyofanyika katika kituo cha GAPCO Kamata jijini Dar es Salaam alisema: "kuanzishwa kwa programu ya GAPCO Safari kutasaidia kutatua changamoto za muda mrefu zinazowakabili wamiliki wa magari nchini. Mfumo huu ni muhimu kuelekea jamii ya kufanya malipo bila fedha taslimu.”
Slaa alipongeza GAPCO kwa kuwa Kampuni ya kwanza katika sekta ya mafuta Kurudisha thamani ya fedha kwa wateja wake nakuomba Kampuni zingine kufuata nyayo za GAPCO.Alibainisha kuwa huduma hii itasaidia kupunguza kwa ujumla, gharama za mafuta, kupunguza bugudha ya makaratasi na kusaidia kuendesha biashara kwa ufanisi zaidi.
Slaa aliongeza kwamba maendeleo kama hayo ni muhimu katika kuboresha uchumi wa nchi kwa kuwa usafiri ni moja ya nguzo muhimu ya uchumi wa Tanzania. Slaa alisisitiza kuwa Serikali itaendelea kuunga mkono juhudi hizo ili kuboresha sekta ya usafiri nchini.Dr Macharia Irungu, Afisa Mtendaji Mkuu (CEO) GAPCO Group alisema GAPCO ina maslahi mapana katika soko la Afrika Mashariki na inajivunia kuwa na vituo vya mafuta 63 nchi nzima, na kuifanya GAPCO kuwa moja ya kampuni ya mafuta inayoongoza.
Akimkaribisha Mgeni Rasmi kuzindua rasmi mpango, Bw. Ashok Dhar, Rais wa Reliance Industries Limited India, kampuni mama ya GAPCO Tanzania Ltd, alisema kuwa mpango huu unawakilisha sehemu ndogo ya faida ya GAPCO.Bw. Dhar alisema anaimani na Uchumi wa Tanzania, na hivyo kampuni yake itaendelea kuwekeza zaidi nchini kwa miaka ijayo.
Akifafanua zaidi juu ya programu ya GAPCO Safari, Vijay Nair, Afisa Uendeshaji (COO) alisema kuwa kadi za Gapco Safari zitakuwa zinapatikana wakati wowote katika vituo vya mafuta vya GAPCO mkoani Dar Es Salaam kwa kuanzia.mtendaji alieleza kuwa huduma hiyo ilikuwa wazi kwa wamiliki binafsi, kampuni na wafanya biashara ya magari.
"Tunataka kuboresha zaidi huduma zetu za uuzaji mafuta kwa wateja wetu. GAPCO tunaandhisha huduma ya kutoa huduma aminifu ambayo ni suluhisho kwa wamiliki wa magari nchini kote… Hii ni huduma ya kipekee tuliyo ianzisha tukiamini kupitia Kauli mbiu ‘……….’," alisema Bw Nair.

Thursday, 20 November 2014

SERIKALI YA MAPINDUZI IMETIMIZA WAJIBU WAKE

MAPEMA WIKI ILIO PITA SERIKALI YA MAPINDUZI ZITOD IMEMPINDUA ALIEKUWA RAISI WA SERIKALI YA WANAFUNZI WA CHUO CHA MAENDELEO YA UTALII ZANZIBAR MH FAHIM NASSOR ALI BAADA YA SKENDO MOTO NA KUMTEUA MH: SHEWEJI MOH'D SHEWEJI KUWA KAIMU RAISI WA CHUO CHA MAENDELEO YA UTALII NA KUTOA TAMKO KUWA ASIEWAJIBIKA MKONDO UTAMKUTA MUANDISHI WAKO ABDUL-LATIF (MATARGIDE) ALIKUWA LIVE KATIKA TOKIA LA KUAPISHWA RAISI HUYO










Wednesday, 19 November 2014

Wabunge waomba muongozo wa spika kuweka muda kujadili taarifa ya PAC kuhusu kashfa ya shilingi Bilioni 200 ya akaunti ya ESCROW.


Wabunge waomba muongozo wa spika kuweka muda kujadili taarifa ya PAC kuhusu kashfa ya shilingi Bilioni 200 ya akaunti ya ESCROW.
Baadhi ya wabunge wameomba mwongozo wa spika unaotaka kamati ya uongozi kweka muda wa kusitisha kujadili taarifa ya kamati ya PAC kuhusu sakata la wizi wa fedha katika akaunti Tegeta ESCROW bada ya kuona utaratibu uliopo unatoa muda mchache wa kujadili  hivyo kufunya uhuru wa wabunge kujadilisha taarifa inayowasilishwa na kamati.
Akiomba mwongozo kwa naibu spika, mbunge wa mtera Mhe.Livingstone Lusinde ametaka kamati ya uoungozi kuongeza muda wa kujadili tuhuma zinazojitokeza na hasa zinagusa baadhi ya mawaziri na wabunge wenyewe ambao wanalalamikiwa.
 
Katika hatua nyingine kamati ya kudumu ya bunge ya uchumi,viwanda na biashara ikitoa maoni kuhusu mswada wa marekebisho ya sheria ya ubia baina ya sekta ya umma na sekta binafsi wa mwaka 2014 imesema changamoto zinazoikabili serikali ni kutokuwepo kwa sera zinazowalinda wazawa kushiriki katika uwekezaji nchini. 
 
Wakichangia muswada wa marekebisho ya sheria ya ubia na bina ya sekta ya umma na sekta binafsi,baadhi ya wabunge wamehoji serikali inampango gani wa kuwawezesha wawekaji wa ndani kama ambavyo nchi nyingine zinazoendelea na zisizoendela zinafanya katika kuwajengea uwezo watu wake.
 
Awali akiwasilisha muswada huo waziri wa nchi ofisi ya waziri mkuu uwekezaji na uwezeshaji, Mhe.Mary Nagu amesema mapendekeza hayo yanalenga kuongeza utekelezaji wa miradi ya ubia pamoja na mazingira yatakayowezesha sekta binafsi kushiriki kikamilifu katika kuwekeza katika miradi ya kiuchumi na kijamii.