Habari kutoka mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo zinasema kuwa, raia waliokuwa wamekimbia makazi yao kufuatia oparesheni ya jeshi la serikali dhidi ya waasi wa FDLR wameanza kurejea nyumbani baada ya miji kadhaa kukombolewa na jeshi hilo. Habari zinasema wakazi wa mji wa Mulenge ulioko katika mkoa wa Kivu Kusini tangu usiku wa jana wameanza kurejea kwenye nyumba zao baada ya mji huo kukombolewa na jeshi la serikali kutoka mikononi mwa FDLR.
Serikali ya DRC ilianzisha oparesheni kali dhidi ya kundi la FDLR linalowajumuisha waasi wa Kihutu wa kutoka Rwanda wanaopiga kambi mashariki mwa Kongo-Kinshasa. Oparesheni hiyo ilianza siku kadhaa zilizopita baada ya waasi hao kukataa kuweka silaha chini na kujisalimisha kwa hiari. Jeshi la kulinda amani la Umoja wa Mataifa huko DRC MONUSCO ambalo awali lilitarajiwa kusaidiana na wanajeshi wa serikali limekataa kushiriki kwenye oparesheni hiyo
No comments:
Post a Comment