Unordered List


Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Thursday, 26 February 2015

Utumiaji mbaya wa intaneti, changamoto kwa TZ

Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia wa Tanzania, Prof. Makame Mbarawa amesema kuwa, utovu wa maadili kupitia intaneti katika nchi yake ni changamoto kubwa kwa serikali ya Dar es Salaam. Akizungumza kwenye mahojiano maalum na Idhaa hii, Waziri Mbarawa amesema katika kutatua tatizo hilo, serikali imepitisha sheria ya kukabiliana na uhalifu wa mitandao ikiwa ni pamoja na kuwabana wanaotumia mtandao kueneza mambo yanayokinzana na maadili kama vile kupakuwa na kusambaza picha za uchi na filamu za ngono. Kuhusiana na kutumiwa teknolojia katika kutatua matatizo ya kisiasa nchini Tanzania na barani Afrika kwa ujumla, Prof. Makame Mbarawa amesema teknolojia ina nafasi ya aina yake katika kupunguza matatizo yanayojitokeza hususan nyakati za uchaguzi katika nchi za Kiafrika. Amesema maandalizi ya chaguzi mbalimbali barani Afrika kuanzia usajili wa wapigakura, upigaji kura, kuhesabiwa kura na kutangazwa matokeo kunaweza kurahisishwa na kuboreshwa zaidi kupitia teknolojia za kisasa na hivyo kuepusha ghasia na machafuko yanayoshuhudiwa katika nchi za Kiafrika baada ya chaguzi hizo.

No comments:

Post a Comment