Unordered List


Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Wednesday, 13 December 2017

Sehemu ya ndege ye jeshi la Marekani imeanguka kwenye shule katika kisiwa cha Okinawa nchini Japan na kuzua upya misukosuko na watu wa eneo hilo.


 Sehemu ya ndege ye jeshi la Marekani imeanguka kwenye shule katika kisiwa cha Okinawa nchini Japan na kuzua upya misukosuko na watu wa eneo hilo.
Sehemu hiyo ya dirisha ilianguka kwenye uwanja wa shule na kusabisha majeraha madogo kwa mwanafunnzi mmoja.
  • Mtu aliyeundia ndege juu ya paa la nyumba yake India
Kisiwa cha Okinawa kina kambi kuwa zaidi ya jeshi la Marekani nchini Japan.
Haki miliki ya picha Hulton Archive
Image caption Sehemu ya helikopta ya jeshi la Marekani yaanguka shuleni Japan
Katika miaka ya hivi karibuni, ajali kadha na visa vya uhalifu vimesababisha kuwepo upinzani dhidi ya kambi hiyo ya Marekani.
Jeshi la Marekani lilithibitisha kuwa dorisha kutoka moja ya helikopta zake ilianguka kwenye uwanja wa michezo wa shule iliyo nje ya kambi ya yake ya jeshi la wanahewa.
Haki miliki ya picha Reuters
Image caption Gavana wa Okinawa Takeshi Onaga aonyesha picha ya dirisha iliyoanguka shuleni